Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chongolo ateuliwa mkuu wa mkoa Songwe
Habari za SiasaTangulizi

Chongolo ateuliwa mkuu wa mkoa Songwe

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo
Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM, Daniel Godfrey Chongolo kuwa mkuu wa mkoa wa Songwe. Chongolo amechukua nafasi ya Dk. Fransis Michael ambaye amewekwa kando. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chongolo aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza chini ya Raisi Samia Suluhu Hassan kuanzia mwaka 2021 hadi 2023 alipojiuzulu, amewahi kuhudumu kama Mkurugenzi wa Mawasiliano chini ya Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo ikiwa chini ya Nape Nnyauye.

Mwaka 2016 aliteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Wilaya ya Loliondo. Mwaka 2018 akahamishiwa Kinondoni kwa wadhifa huo huo wa ukuu wa wilaya.

Chongolo amewahi kushika nafasi zingine kama vile Mhariri wa Radio Uhuru inayomilikiwa na CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!