WACHEZAJI wawili wa kikosi cha Simba, Clatous Chama na Luis Miquisone wameingia kwenye kikosi cha kwanza cha wiki barani Afrika. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Kikosi hiko ambacho kina wachezaji 11, ambao wamefanya vizuri kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika katika michezo ya makundi iliyopigwa hivi karibuni.
Wachezaji hao wameingia kwenye kikosi hiko baada ya kuonesha kiwango kizuri kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa ambapo Simba iliminyana dhidi ya AS Vita kutoka Jamhuri ya Congo.
Kwenye mchezo huo wa kundi A, uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa Simba walifanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 4-1 na kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Katika ushindi huo wa mabao 4-1, wachezaji hao wawili walihusika moja kwa moja kwenye mabao hayo manne.
Chama alifanikiwa kufunga mabao mawili na kutoa pasi ya goli moja (assist), huku Miquisone akiingia kambani mara moja.
Wakati huo huo, Chama amewekwa kwenye kinyang’anyiro cha mchezaji bora wa wiki pamoja na wachezaji Ricardo Goss wa Mamelodi Sundown, Amir Sayoud wa CR Belouizdad na Ferjani Sassi.
Katika kinyang’anyiro hiko Chama anaongoka akiwa na asilimia 51 baada ya kupigiwa kura nyingi kuliko wengine.
Leave a comment