Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia afungulia vyombo vya habari
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia afungulia vyombo vya habari

Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameiagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuvifungulia vyombo vyote vya habari vilivyofungiwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Samia ametoa agizo hilo leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, Ikulu ya Dar es Salaam, mara baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni.

Akigusia sekta ya habari, Rais Samia amesema “wizara ya habari, mnapaswa kusimamia vyombo vya habari, nasikia kuna vyombo vya habari huko mmevifungia, vifungulieni lakini vifuate sheria na kanuni.”

Rais Samia amesema, “tusiwape mdomo mdomo wa kusema tunabinya uhuru wa habari na nataka kanuni ziwe wazi, ili mtu akifungiwa ajue kosa na adhabu yake. Tusifungie tu kibabe.”

Baadhi ya magazeti yaliyofungiwa ni; MwanaHALISI, Mawio, Tanzania Daima na Mseto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!