Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yataka Serikali kutumia mbinu za kisayansi kudhibiti uvamizi wanyama pori
Habari za Siasa

Chadema yataka Serikali kutumia mbinu za kisayansi kudhibiti uvamizi wanyama pori

Mbowe akihutubia wananchi
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Serikali kutumia mbinu za kisayansi kudhibiti uvamizi wa wanyamapori katika maeneo wanaoyoishi wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 30 Agosti 2023 na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, akizungumza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho, kwenye Jimbo la Kisesa, mkoani Simiyu.

“Wale wanyama wanafuta mlo, kwa bahati mbaya wanaishi jirani na makazi ya watu. Tatizo sio la wanyamapori wala wananchi, tatizo ni viongozi wa Serikali walioshindwa kutengeneza mikakari na mbinu za kuwadhibiti wanyama ili waishi katika mahusiano mema na jamii ya wananchi waliopakana na hifadhi,” amesema Mbowe.

Mbowe ameitaka Serikali kuiga mfano kutoka nchi jirani zenye mbuga za wanyamapori, wanaotumia mbinu za kisayansi ikiwemo kujenga kuta za umeme.

“Nimesema sera ya CCM kuhusu kudhibiti kuhama na kuhifadhi wanyama hakujafanyika kisayansi, kunafanyika kama vile wakati Mungu anaumba dunia. Maisha ya leo sayansi inakwenda mbele sana na chukua mfano wa Kenya ukienda hutakuta hata siku moja anatoka fisi anawaumiza wananchi sababu wameweka mfumo wa kuwalinda raia kwa kuweka fensi za umeme,” amesema Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!