CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Serikali kutumia mbinu za kisayansi kudhibiti uvamizi wa wanyamapori katika maeneo wanaoyoishi wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu…(endelea).
Wito huo umetolewa leo tarehe 30 Agosti 2023 na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, akizungumza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho, kwenye Jimbo la Kisesa, mkoani Simiyu.
“Wale wanyama wanafuta mlo, kwa bahati mbaya wanaishi jirani na makazi ya watu. Tatizo sio la wanyamapori wala wananchi, tatizo ni viongozi wa Serikali walioshindwa kutengeneza mikakari na mbinu za kuwadhibiti wanyama ili waishi katika mahusiano mema na jamii ya wananchi waliopakana na hifadhi,” amesema Mbowe.
Mbowe ameitaka Serikali kuiga mfano kutoka nchi jirani zenye mbuga za wanyamapori, wanaotumia mbinu za kisayansi ikiwemo kujenga kuta za umeme.
“Nimesema sera ya CCM kuhusu kudhibiti kuhama na kuhifadhi wanyama hakujafanyika kisayansi, kunafanyika kama vile wakati Mungu anaumba dunia. Maisha ya leo sayansi inakwenda mbele sana na chukua mfano wa Kenya ukienda hutakuta hata siku moja anatoka fisi anawaumiza wananchi sababu wameweka mfumo wa kuwalinda raia kwa kuweka fensi za umeme,” amesema Mbowe.
Leave a comment