Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apangua tena Manaibu Mawaziri, Mnyeti ahamishwa kabla ya kuapishwa
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia apangua tena Manaibu Mawaziri, Mnyeti ahamishwa kabla ya kuapishwa

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya
uhamisho na uteuzi wa viongozi mbalimbali ikiwamo Naibu Waziri David Silinde ambaye amehamishwa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenda kuwa Naibu Waziri wa Kilimo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Sakaam …(endelea).

Aidha, Alexander Mnyeti ambaye mapema leo ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, jioni hii amehamishiwa katika nafasi ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi.

Katika taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu leo Jumatano jioni, pia Rais Samia amemteua Balozi Mhandisi Aisha Amour kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi.

Katika taarifa hiyo pia ameteua Wajumbe wanne wa Tume ya Mipango.

Wajumbe hao ni Balozi Ombeni Yohana Sefue – Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu na Omar Issa – Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela.

Wengine ni Balozi Ami Ramadhan Mpungwe – Balozi Mstaafu na Mịasiriamali na Maryam Salim- Mencja Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Cambodia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!