RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya
uhamisho na uteuzi wa viongozi mbalimbali ikiwamo Naibu Waziri David Silinde ambaye amehamishwa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenda kuwa Naibu Waziri wa Kilimo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Sakaam …(endelea).
Aidha, Alexander Mnyeti ambaye mapema leo ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, jioni hii amehamishiwa katika nafasi ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi.
Katika taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu leo Jumatano jioni, pia Rais Samia amemteua Balozi Mhandisi Aisha Amour kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi.
Katika taarifa hiyo pia ameteua Wajumbe wanne wa Tume ya Mipango.
Wajumbe hao ni Balozi Ombeni Yohana Sefue – Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu na Omar Issa – Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela.
Wengine ni Balozi Ami Ramadhan Mpungwe – Balozi Mstaafu na Mịasiriamali na Maryam Salim- Mencja Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Cambodia.
Leave a comment