Saturday , 30 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaandaa mpango Watanzania kutumia Shilingi China
Habari Mchanganyiko

Serikali yaandaa mpango Watanzania kutumia Shilingi China

Spread the love

NAIBU Waziri wa Fedha, Hamadi Chande amesema serikali inatarajia kuja na mpango wa kuwezesha wafanyabiashara wa Tanzania na China kutumia sarafu ya Tanzania kununua bidhaa nchini China. Anaripoti Maryam Mudhihiri na Mlelwa Kiwale…(endelea).

Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande ameyasema hayo leo tarehe 30 Agosti 2023, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Cosato Chumi (CCM) aliyetaka kufahamu iwapo serikali ipo tayari kuandaa mazingira ya kuwezesha biashara kati ya China na Tanzania kufanyika kwa shillingi.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo, amesema kuwa serikali itaifanyia kazi jambo hilo ili kuona ni nini kinafanyika kuwezesha bishara ya China kukubali matumizi ya sarafu ya Tanzania.

“Katika biashara za kitaifa wafanyabiashara wanaouhuru wa kutumia sarafu yoyote inayorahisisha biashara zao inayokubalika na nchi nyingine kwa lengo la kupunguza gharama za miamala na muda,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!