Sunday , 12 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaandaa mpango Watanzania kutumia Shilingi China
Habari Mchanganyiko

Serikali yaandaa mpango Watanzania kutumia Shilingi China

Spread the love

NAIBU Waziri wa Fedha, Hamadi Chande amesema serikali inatarajia kuja na mpango wa kuwezesha wafanyabiashara wa Tanzania na China kutumia sarafu ya Tanzania kununua bidhaa nchini China. Anaripoti Maryam Mudhihiri na Mlelwa Kiwale…(endelea).

Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande ameyasema hayo leo tarehe 30 Agosti 2023, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Cosato Chumi (CCM) aliyetaka kufahamu iwapo serikali ipo tayari kuandaa mazingira ya kuwezesha biashara kati ya China na Tanzania kufanyika kwa shillingi.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo, amesema kuwa serikali itaifanyia kazi jambo hilo ili kuona ni nini kinafanyika kuwezesha bishara ya China kukubali matumizi ya sarafu ya Tanzania.

“Katika biashara za kitaifa wafanyabiashara wanaouhuru wa kutumia sarafu yoyote inayorahisisha biashara zao inayokubalika na nchi nyingine kwa lengo la kupunguza gharama za miamala na muda,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!