Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yataka mambo 4 marekebisho sheria za uchaguzi
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yataka mambo 4 marekebisho sheria za uchaguzi

John Mnyika
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewasilisha mapendekezo makuu manne mbele ya Kamati ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, juu ya miswada ya  marekebisho ya sheria za uchaguzi, iliyowasilishwa na Serikali bungeni jijini Dodoma Novemba 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mapendekezo hayo yamewasilishwa leo tarehe 10 Januari 2024 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, mbele ya kamati hiyo bungeni jijini Dodoma baada ya wadau mbalimbali ikiwemo Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (THRDC), kuwasilisha kuwasilisha maoni yao.

Pendekezo la kwanza lililowasilishwa na Chadema ni Serikali kuondoa bungeni miswada hiyo kwa madai kuwa haijajibu matatizo ya msingi ya muundo wa tume ya taifa ya uchaguzi wala sheria za uchaguzi, wakati la pili likiitaka Serikali iwasilishe bungeni muswada wa kukwamua mchakato wa upatikanaji katiba mpya.

Wapiga kura

Pendekezo la tatu, ni Serikali iwasilishe bungeni muswada wa kufanya marekebisho ya mpito ya katiba ya sasa ili kuwezesha upatikanaji wa chaguzi huru na za haki baada ya kuondoa vifungu vya kikatiba vyenye mapungufu.

La mwisho ni, Serikali kupeleka muswada wa sheria itakayowezesha tume ya taifa ya uchaguzi kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa badala ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Chadema kimetaja maeneo ya katiba yenye mapungufu ambayo yanatakiwa kurekebishwa ili kuboresha mfumo wa uchaguzi, ikiwemo Ibara ya 39 (2) ya katiba, ili kuondoa ulazima wa mtu kuwa mwanachama wa chama cha siasa ndipo awe na sifa za kugombea nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Chama hicho kimependekeza ibara ya 41(7) ya katiba ifanyiwe marekebisho ambayo inakataza matokeo ya urais kuhojiwa mahakamani, ili wapiga kura au wagombea wawe na haki ya kuhoji matokeo hayo kwenye Mahakama ya Rufani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!