Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CDF aonya ongezeko vijana kujiunga vikundi vya kigaidi, wakimbizi kuingia serikalini
Habari za Siasa

CDF aonya ongezeko vijana kujiunga vikundi vya kigaidi, wakimbizi kuingia serikalini

Spread the love

MKUU wa Majeshi nchini (CDF), Jenerali Jacob Mkunda, amesema kuna tishio la ongezeko la vijana wa kitanzania kujiunga na vikundi vya kigaidi katika mataifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Msumbiji na Somalia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

CDF Mkunda ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari 2024, katika mkutano wa saba kati yake na makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), jijini Dar es Salaam, ambao umefunguliwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

“Hali ya ulinzi na usalama ndani ya nchi kwa ujumla ni shwari licha ya uwepo wa matishio ya kiusalama hasa tishio la kiugaidi na itikadi kali, wana mtandao wa kigaidi wamekuwa wakiwaunganisha vijana wetu wenye umri wa miaka kati ya 15 na 35, kisha kuwasafirisha kwenda kujiunga na makundi ya kigaidi. Hali hii inaonyesha upo ukuaji wa tatizo hilo hapa nchini,” amesema CDF Mkunda.

Katika hatua nyingine, CDF Mkunda amesema katika mikoa ya Tanzania upande wa magharibi, inakabiliwa na changamoto ya ongezeko la wakimbizi na waomba hifadhi wa muda mrefu kutoka Burundi, Rwanda, DRC, kitendo kinachohatarisha usalama wa nchi kwa kuwa baadhi yao wanafanya njama kuhakikisha wanapata uraia na nafasi nyeti za uongozi serikalini.

“Waomba hifadhi bado wanaendelea kuishi vijijini na kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha uzao wao unapata uraia wa Tanzania bila kufuata sheria. Kuanzia Januari hadi Disemba 2023 watu 138149, waomba hifadhi walipokelewa Tanzania na kutokana na mahojiano wamebainika wamekuja kwa sababu za kiuchumi na zinawakosesha sifa ya kupewa hadhi ya ukimbizi,” amesema CDF Mkunda.

Amesema “Ni maoni yetu kwamba, kuendelea kuwepo kwa muda mrefu kwa waomba hifadhi na wakimbizi nchini ni tishio la kiusalama kwani taarifa zilizopo ni kwamba baadhi ya waomba hifadhi au familia zao wameajiriwa serikalini kwa nafasi mbalimbali na wengine wamepewa teuzi serikalini katika nafasi nyeti za maamuzi.”

CDF Mkunda amesema matishio hayo yameendelea kudhibitiwa kwa ushirikiano wa jeshi na vyombo vingine vya usalama.
Kuhusu hali ya usalama katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji, CDF Mkunda amesema iko shwari baada ya vikosi vya kijeshi vya SADC na vya serikali ya nchi hizo mbili kufanya kazi kubwa.
Aidha, amesema vikosi vya SADC vinatarajiwa kuondoka Machi mwaka huu kitendo kinachoweza hatarisha usalama wa mpaka huo kutokana na kikundi cha kigaidi bado kuendelea kuwa na nguvu.
Akizungumzia mkutano huo, CDF Mkunda amesema utafanyika kwa muda wa siku tano ambapo lengo lake ni kujadili namna ya makanda hao kutekeleza majukumu yao ya msingi ya ulinzi wa nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

error: Content is protected !!