Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM :Hatutaki ushindi wa makandokando uchaguzi Serikali za mitaa
Habari za Siasa

CCM :Hatutaki ushindi wa makandokando uchaguzi Serikali za mitaa

Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakihitaji ushindi wa makandokando katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na kwamba kinajipanga kuandaa wagombea bora pamoja na kuongeza idadi ya wapiga kura ili kishinde kwa misingi ya kidemokrasia. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza katika mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM, Emanuel Nchimbi na viongozi wa chama hicho Mkoa wa Katavi, leo Jumamosi, Katibu wa Oganaizesheni CCM, Issa Gavu, amesema uchaguzi wao ni wa kidemokrasia ambao unakwenda na hesabu ya wingi wa kura za wananchi.

“Katika uchaguzi wa wenyeviti wa vijiji, kitongoji ama mtaa tunachohitaji CCM ni ushindi, hatuhitaji ushindi unaotokana na makandokando tunahitaji ushindi unaotokana na wagombea wenye sifa na utayari wa kupeperusha bendera ya chama chetu. Tukipendekeza wagombea wazuri hatuna sababu ya kuendekeza rushwa wala kuendekeza wachache wasiotaka maslahi ya wengi,” amesema Gavu.

Aidha, Gavu amesema CCM kinawaonya wabunge na madiwani wenye tabia ya kupanga safu za viongozi wa serikali za mitaa kupitia uchaguzi huo, huku akiwatahadharisha wajumbe kutopitisha wagombea wenye makandokando.

“Tunayo nafasi ya kupima viongozi wetu wenye dhamira kugombea, uongozi wa wilaya ndio tumewapa majukumu ya katiba kutuorodheshea wagombea wa nafasi za wenyeviti wa vijiji, mitaa na vitongoji tunawaomba hakikisheni haki inatendeka acheni kupanga safu kwa kuogopa madiwani na wabunge, pangeni safu ya ushindi,” amesema Gavu.

Gavu amesema “ tunataka tuhakikishe kwamba kila mgombea anayetoka CCM hatupati mwenye makandokando tunataka mgombea yuko safi akikwekwa asubuhi tayari saa nne CCM tumeshinda. Tukikumbatia watu wenye makandokando likitajwa tatizo la ardhi mwenyekiti yumo huyo hana nafasi ndani ya CCM.”

Gavu amewataka wanachama wa CCM kuongeza juhudi za kupata wanachama wapya pamoja na kuwahimiza kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwani ndio njia pekee ya kupata ushindi “idadi ya wana CCM iwe nyingi na kubwa maana yake ushindi wa chama chetu utakuwa wa wazi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

error: Content is protected !!