Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CAG abaini madudu CCM, Chadema
Habari za Siasa

CAG abaini madudu CCM, Chadema

Spread the love

 

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere amebaini uidhinishaji na uhakiki wa malipo ya Sh.797.2 milioni uliofanywa na Chama Cha Mapinduzi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) bila kufuata taratibu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea). 

Ripoti hiyo ni yam waka 2020/21 inayoishia Juni 2021 ambayo leo Jumanne, tarehe 12 Aprili 2022 imewasilishwa bungeni jijini Dodoma na baadaye CAG Kichere amezungumza na waandishi wa habari.

CAG amesema Afisa Masuuli wa chama cha siasa pamoja na mambo mengine anatakiwa kuhakikisha taratibu za fedha za chama chake zinafuatwa kwa namna ambayo rasilimali za chama hicho zitalindwa.

Amesema miongozo ya taratibu za kifedha inayotumiwa na vyama vya siasa inamtaka Afisa Masuuli kupitia, kuchunguza, kukagua na kuidhinisha malipo au shughuli yoyote inayotekelezwa na Chama chake.

Ofisi ya Chadema Makao Makuu, Dar es Salaam

CAG Kichere amesema, ili kufikia lengo hilo, CCM kilianzisha Kitengo cha uhakiki, ambacho humsaidia Afisa Masuuli katika jukumu la kukagua malipo ya awali kabla ya kibali cha mwisho kutolewa.

“Pamoja na kuwa na kitengo cha uhakiki, niligundua kuwa CCM kililipa Sh. milioni 786.44 bila ya kufanyiwa ukaguzi wa awali na kuidhinishwa na Afisa Masuuli,” amesema

Aidha, amesema “nilibaini kuwa Chadema kililipa Sh. milioni 9.75 bila ya kuwa na kibali cha Afisa Masuuli.”

Amesema, kutokana na dosari hizo zilizobainika, kuna hatari ya rasilimali za vyama kutumika vibaya iwapo malipo yataendelea kufanyika mara kwa mara, bila kupata kibali kutoka kwa Maafisa Masuuli.
“Kwa maana hiyo, ninapendekeza uongozi wa CCM na Chadema kusimamia udhibiti wa ndani ili malipo yasifanyike bila ya kuwa na kibali cha Afisa Masuuli,” amesema CAG Kichere

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

error: Content is protected !!