Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lamkana Mbowe nyongeza ya mishahara
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamkana Mbowe nyongeza ya mishahara

Spread the love

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limekanusha madai ya taarifa kwamba mwaka jana wabunge wamejiongezea mishahara kutoka Sh 13 milioni hadi Sh 18 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kudai katika mkutano wake wa hadhara Mjini Babati Mkoani Manyara kuwa wabunge hao wamejiongezea kiasi hicho cha mshahara.

Taarifa hiyo ya Mbowe ilisambaa katika mitandao ya kijamii kwa njia ya video na kuibua mjadala kuhusu uweledi wa wawakilishi hao wa wananchi hasa ikizingatiwa makundi mbalimbali ya watumishi wa umma wanalia mishahara kiduchu wanayolipwa na Serikali.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa leo Jumamosi na Kitengo cha Bunge cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa imesema madai hayo ni uzushi na upotoshaji .
“Hakuna Mbunge aliyeongezewa mshahara kama alivyodai. Hivyo, tunapenda kuwashauri na kuwasihi wananchi kupuuza madai hayo ambayo lengo lake ni kuleta taharuki pamoja na kuwagombanisha wananchi na wawakilishi wao.

“Nyongeza ya mshahara ni suala linalozingatia bajeti na hakuna utaratibu wa aina
yoyote kama huo ambao umefanyika kwa ajili ya kuwaongezea waheshimiwa wabunge mishahara,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!