Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bawacha yasitisha kongamano la siku ya wanawake duniani
Habari za Siasa

Bawacha yasitisha kongamano la siku ya wanawake duniani

Sharifa Suleiman, Makamu wa Bawacha-Zanzibar
Spread the love

 

BARAZA la Wanawake wa Chama cha Demokarasia na Maendeleo (Bawacha), nchini Tanzania, limesitisha kongamano la ‘Siku ya Wanawake Duniani’ kitaifa, lililopangwa kufanyika mkoani Iringa, 8 Machi 2021. Anaripoti Matrida Peter, Dar es Salaam … (endelea).

Sababu zilizosababisha kuahirishwa kwa kongamano hilo, ni kuzuia maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

Uamuzi wa kuahirisha, ulifikiwa jana Jumatatu tarehe 1 Machi 2021, katika kikao cha kamati ya utendaji ya Bawacha, iliyokutana kwa njia ya mtandao.

“…imefikia uamuzi huo, ikiwa ni jitihada mojawapo ya kuzuia maambukizi ya virusi vya corona, vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19 (matatizo kwenye mfumo wa hewa wa binadamu), yanayosababisha vifo kwa wapendwa wetu,” amesema Sharifa Suleiman, makamu wa Bawacha-Zanzibar, kupitia taarifa yake kwa umma

Amesema, zaidi ya wanawake 3,000, kutoka mikoa mbalimbali nchini, walikuwa wamethibitisha kushiriki hivyo, itakuwa vigumu kuepuka msongamano, kutokana na tukio lenyewe.

Sharifa amesema, hali itakaporuhusu mkusanyiko mkubwa kama huo, Bawacha itatangaza mahali na tarehe rasmi ya kungamano jingine maalum ambalo, litakutanisha wanawake wote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!