Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Morrison aachwa safari ya Sudan
Michezo

Morrison aachwa safari ya Sudan

Bernard Morrison
Spread the love

 

KLABU ya Simba itaondoka nchini leo kuelekea Khartoum, Sudan kuwavaa El Merreikh kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaopigwa tarehe 6 Machi 2021, huku jina la mchezaji Bernard Morrison likikosekana kwenye orodha ya wachezaji watakaosafiri. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Simba itaondoka na wachezaji 25, kupitia Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere majira ya saa 10:45 jioni na Shirika la Ndege la Ethiopia na watawasili nchini Sudan kesho mchana.

Morrison ameachwa kutokana na kuwa majeruhi baada ya kuumia katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Biashara United uliopigwa kwenye Uwanja wa Karume, Mara.

Simba inaenda kucheza mchezo huo huku ikiwa imefanya vizuri kwenye michezo miwili ya awali na kujiokotea pointi sita baada ya kuwafunga AS Vita na Al Ahly.

Mpaka sasa kwenye kundi A, Simba wanashikilia nafasi ya kwanza wakiwa na pointi 6 baada ya kucheza michezo miwili, huku nafasi ya pili ikishikwa na AS Vita akiwa na pointi tatu sawa na Al Ahly nafasi ya mwisho inashikwa na El Merreikh ambayo haina pointi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!