Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bandari ya Kigoma yaipiku Mwanza
Habari za SiasaTangulizi

Bandari ya Kigoma yaipiku Mwanza

Bandari ya Kigoma
Spread the love

 

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusidedit Kakoko amesema, maboresho makubwa yaliyofanywa katika Bandari ya Kigoma yameanza kuleta matokeo chanya ikiwemo kuongezeka kwa shehena ya mizigo pamoja na mapato. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jana Ijumaa tarehe 5 Machi 2021, katika Bandari ya Kigoma, Mhandisi Kakoko alisema, shehena na mapato katika bandari hiyo yameongezeka kiasi cha kuipiku Bandari ya Mwanza ambayo ndiyo iliyokuwa ikiongoza kabla ya maboresho hayo.

Alisema, Bandari ya Kigoma ambayo inahusisha bandari zote zilizopo Ziwa Tanganyika, imeanza kufanyiwa maboresho kuanzia mwaka 2016/17, ikihusisha ujenzi wa magati, ununuzi wa mitambo, ujenzi wa maghala na majengo ya abiria pamoja na ujenzi wa ofisi za kisasa za makao makuu ya bandari hiyo ambazo ziko katika hatua za mwisho kukamilika.

Mkurugenzi huyo alisema, maboresho hayo, yalisukumwa na kasi kubwa ya ongezeko la mahitaji ikilinganishwa na miundombinu iliyokuwepo.

Alisema bandari za Ziwa Tanganyika zimekuwa kiungo kikubwa cha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani za DRC, Burundi na Zambia, biashara kubwa ikiwa ni mazao yanayozalishwa Tanzania.

Kutokana na hali hiyo alisema, bandari hizo zimekuwa kichocheo kikubwa cha kukuza uchumi wa wananchi wa mikoa inayozunguka Ziwa Tanganyika kwani mazao yao yanapata wanunuzi wengi wanaovutiwa na maboresho ya bandari.

Alisema, bandari hizo pamoja na kuanza kazi kwa reli, kumesaidia kupunguza bei za bidhaa ambazo husababishwa na gharama kubwa za usafirishaji.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (PTA), Mhandisi Deusidedit Kakoko

Alisema bado kuna maboresho zaidi yanaendelea katika bandari Kuu ya Kigoma yanahusisha ujenzi wa gati ya maboti ya Kibirizi, gati ya abiria na makasha na ujenzi wa bandari Kavu ya Katosho.

“Tumekusudia kuifanya bandari ya Kibirizi na Kigoma kuwa ya mizigo ya nje na ile ya Katosho itakuwa ya ndani, ” alisema Kakoko.

Alisema matarijio ya kuongezeka zaidi kwa shehena na abiria ni makubwa kutokana na maboresho ya meli yanayotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Huduma za Meli zikiwemo MV Mwongozo, MV Liemba na MT Sangara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!