KAMATI ya Halmshauri Kuu ya CCM leo Jumatatu imemteua Balozi Emmanuel John Nchimbi (53) kuwa Katibu Mkuu wa CCM akichukua nafasi ya Daniel Chongolo aliyejiuzulu tarehe 28 Novemba mwaka jana. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Nchimbi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri kabla ya kumaliza muda wake. Awali alikuwa mbunge wa Songea mjini (CCM) kuanzia mwaka 2010 hadi 2015 pia alikuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi.
Balozi Dk. Nchimbi ameteuliwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan aliyeongoxa kikao maalumu cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya chama hicho kilichofanyika leo Jumatatu mjini Unguja, Zanzibar.
Leave a comment