Saturday , 30 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi Ali Idi Siwa bosi mpya usalama wa Taifa
Habari za SiasaTangulizi

Balozi Ali Idi Siwa bosi mpya usalama wa Taifa

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameendelea kupangua Idara ya Usalama wa Taifa baada ya leo Jumatatu kumteua Balozi Ali ldi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Balozi Ali Idi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti 2023.

Balozi Siwa amechukua nafasi ya Said Hussein Massoro ambaye amehudumu kwenye nafasi hiyo kwa miezi saba peke yake kuanzia tarehe 3 Januari mwaka huu.

Balozi Siwa ameapishwa leo tarehe 28 Agosti 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam na kuchukua nafasi ya Said Hussein Massoro ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo, Balozi Siwa alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) nafasi ambayo aliteuliwa na Rais John Magufuli mwaka 2018 kisha mwaka 2021 Rais Samia akamuongezea muda.

Awali kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!