Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi Ali Idi Siwa bosi mpya usalama wa Taifa
Habari za SiasaTangulizi

Balozi Ali Idi Siwa bosi mpya usalama wa Taifa

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameendelea kupangua Idara ya Usalama wa Taifa baada ya leo Jumatatu kumteua Balozi Ali ldi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Balozi Ali Idi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti 2023.

Balozi Siwa amechukua nafasi ya Said Hussein Massoro ambaye amehudumu kwenye nafasi hiyo kwa miezi saba peke yake kuanzia tarehe 3 Januari mwaka huu.

Balozi Siwa ameapishwa leo tarehe 28 Agosti 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam na kuchukua nafasi ya Said Hussein Massoro ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo, Balozi Siwa alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) nafasi ambayo aliteuliwa na Rais John Magufuli mwaka 2018 kisha mwaka 2021 Rais Samia akamuongezea muda.

Awali kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!