Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari Askofu Katoliki afariki dunia, Rais Samia amlilia
Habari

Askofu Katoliki afariki dunia, Rais Samia amlilia

Marehemu Askofu Alfred Maluma wa jimbo katoriki Njombe
Spread the love

 

ASKOFU Alfred Maluma wa Jimbo Katoliki la Njombe nchini Tanzania, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Padri Justin Sapula wa Jimbo Katoliki la Njombe amesema, Askofu Maluma alifikwa na mauti saa 6:40 usiku wa 6 Aprili 2021 na taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Kufuatia kifo hicho, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kwa waumini wa Kanisa Katoliki na wananchi wa Njombe.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia ameandika “nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Askofu wa Jimbo Katoliki la Njombe Mhashamu Baba Askofu Alfred Maluma.”

“Alikuwa mtu mwema, mpenda maendeleo na aliyekuwa tayari kushirikiana na Serikali wakati wote. Nawapa pole Wakatoliki wote, Wananjombe na wote walioguswa na msiba huu,” amesema Rais Samia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!