Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Kufungiwa Mwakalebela, Yanga yaikomalia TFF
Michezo

Kufungiwa Mwakalebela, Yanga yaikomalia TFF

Frederick Mwakalebela, Makamu Mwenyekiti wa Yanga
Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Yanga umesema kuwa haujaridhishwa kufungiwa kwa miaka mitano kwa Makamu Mwenyekiti wao, Fredrick Mwakalebela baada ya kukutwa na hatia na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mwakalebela alifungiwa miaka mitano na kupigwa faini ya shilingi milioni saba, baada ya kukutwa na hatia katika makossa mawili ikiwemo kushindwa kuthibitisha madai ya kuwa vyombo vinavyosimamia mpira wa miguu nchini kuihujumu klabu ya Yanga.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo imeeleza kuwa imepokea kwa mshtuko taarifa hiyo ya kufungiwa kwa kiongozi wao iliyotolewa Ijumaa tarehe 2, machi 2021.

Yanga wamesema kuwa kufungiwa kwa kiongozi huyo ni kama vitisho na kuufunga mdomo uongozi wa Yanga juu ya masuala yake muhimu yaliyowasilishwa TFF.

Aidha taarifa hiyo imendelea kueleza kuwa klabu hiyo inasubiri kupokea taarifa rasmi kutoka TFF ikiwemo hukumu ya shauli hilo ili kukata rufaa na kuchukua hatua nyingine.

Katika taarifa iliyotoka TFF kuhusu kufungiwa kwake ilieleza kuwa Mwakalebela alishindwa kuthibitisha shutuma za kuwa TFF, Bodi ya Ligi na Kamati ya Uendeshaji wa Ligi kuwa inahujumu klabu ya Yanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!