Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu ashauri jopo la wanasheria liundwe kujadili upya mkataba uwekezaji bandari
Habari za Siasa

Askofu ashauri jopo la wanasheria liundwe kujadili upya mkataba uwekezaji bandari

Askofu Anthony Mlyashimba
Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Baptist Kanda ya Kati, Anthony Mlyashimba ametoa wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake kukubali kuufumua mkataba wa uwekezaji wa bandari kwa kuwa unaligawa Taifa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea).

Askofu Mlyashimba ametoa wito huo leo Jumapili tarehe 23 Julai 2023 wakati wa ibada maalumu ya kuliombea Taifa iliyofanyika katika kanisa la Nzuguni Baptist City lililopo Nzuguni jijini Dodoma.

Amesema kuwa kwa sasa taifa limegawanyika kutokana na kuwepo kwa mkataba huo ambao umesababisha taharuki kubwa kwenye jamii.

Amesema ni busara kwa viongozi kuhakikisha mkataba huo unasitishwa mara moja ili kutafuta ufumbuzi ambao utafanya kuwepo kwa umoja, amani, mshikamano na upendo tofauti na ilivyo sasa.

“Kwa sasa nchi imekuwa na pande mbili na kuna watu ambao wanasema bandari imebinafsishwa na wengine wanasema imeuzwa, kumesababisha kuwepo kwa mpasuko ambao unaweza kusababisha makubwa.

“Kwa kuzingatia maneno ya Mungu yanasema katika kitabu cha Zaburi 133 mstari wa kwanza; “Tazama ilivyo vyema na kupendeza ndugu wakae pamoja kwa umoja” kwa hiyo kuna mambo mawili ya kukaa pamoja na umoja lakini mnaweza kukaa pamoja na msiwe na umoja,” amesema.

Aidha, amesema kuna haja ya kuwatafuta wabobezi wa sheria za mikataba na kueleza umma ukweli.

Ameeleza kushangazwa na ukimya wa Prof Paramagamba Kabudu na George Simbachawene ambao ni watalaam wa sharia ndani ya Serikali.

Amesema kusitisha mkataba huo ni afya kwa taifa na kuendelea kushupaza shingo ni kulifanya taifa kuingia katika giza neno ambalo litasababisha matatizo katika kizazi kijacho pamoja na vijukuu kutokana na hali hiyo mkataba uondolewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!