Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Akamatwa kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu na kuiibia maji SHUWASA
Habari Mchanganyiko

Akamatwa kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu na kuiibia maji SHUWASA

Spread the love

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, imemkamata Michael George Clement, mkazi wa Ndala Manispaa ya Shinyanga kwa tuhuma za kuhujumu miondombinu na kuiba maji kinyume cha sheria. Anaripoti Mwandishi Wetu…(Shinyanga).

Clement alikamatwa usiku wa tarehe 3 Septemba 2023 kutokana na uchunguzi uliofanywa na  timu ya SHUWASA kwa kushirikiana na wasamaria wema.

Afisa Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa SHUWASA, Nsianel Gerald

Ni baada ya kutilia shaka matumizi yake ya maji kutoendana na kiasi  cha ankara za mwezi.

Akizunguumza na waandishi wa habari mara baadaya tukio hilo,  Afisa Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma wa SHUWASA, Nsianel Gerald, alisema mtuhumiwa huyo alikuwa anaiba na kuuza maji kinyume cha taratibu na pasipo kibali cha biashara ya maji.

“Tulianza kutilia shaka matumizi yake ya mwezi (bill) baada ya kuonekana ni ndogo ikilinganishwa na biashara ya kuuza maji ambayo nayo alikuwa akiifanya kinyume cha taratibu,” alisema Nsianeli na kuongeza;

“Pamoja na kuuza maji lakini bili yake haikuwahi kuzidi Sh 6,000 kwa mwezi kwa kipindi cha miaka minne na ndipo tukaanza kumfuatilia na kumchunguza na hatimaye usiku wa tarehe 3 Septemba, 2023 tukabaini amechepusha maji kabla ya dira ya maji,” alisema.

Clement anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa taratibu zaidi za kisheria.

Akifafanua kuhusu utaratibu wa kuuza maji alisema, usajili wao ni tofauti na watumiaji wa majumbani na bei zao za maji ni tofauti.

“Mteja wa majumbani hapaswi kuuza maji na kama mtu anataka kuuza maji anapaswa kusajiliwa kama gati la kuuzia maji na bei za maji zinakuwa tofauti,” alisema Gerald.

Aidha, alitoa  wito kwa wananchi kuacha kuhujumu miundombinu ya maji na kuiba maji kwani ni kosa kisheria na adhabu yake ni faini kuanzia Sh. 500,000 hadi Sh Milioni 50 na/au kifungo jela.

Pia aliwasihi wananchi kutoa ushirikiano kwa timu ya SHUWASA kwa kuripoti watu wanaowatilia shaka kuwa ni wezi wa maji ili kuweza kuwafuatilia  na uchunguzi na kuwakamata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!