Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yabariki CCM kumsulubu Zitto
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yabariki CCM kumsulubu Zitto

Spread the love

WAKATI Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakipanga kumsulibu Zitto Kabwe, Chama cha ACT Wazalendo kimebariki mkakati huo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

ACT-Wazalendo kimeshauri Wabunge wa CCM kujipanga kwa hoja kwa kuwa, hoja za Zitto, Kiongozi Mkuu wa chama hicho na Mbunge wa Kigoma Mjini ni zenye kutafitiwa.

Ado shaibu, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT Wazalendo ametoa taarifa ya msimamo wa chama hicho na kusambazwa na Zitto mwenyewe.

Taarifa hiyo inatokana na dhamira ya wabunge CCM kutaka kumkabili Zitto kwa madai ya kumsumbua Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri pia upotoshaji.

Baada ya kukutana kwenye Kamati ya Wabunge wa CCM (Caucus) wamemwona mbunge huyo ni adui namba moja.

Ado na ACT-Wazalendo wanaungana na dhamira ya CCM dhidi ya Zitto ila kwa kupambana kwa hoja.

Amesema, walichopanga kukifanya wabunge wa CCM, bila kujali wanatumia hoja yenye uzito gani kujibu, ndiyo maana hasa ya siasa.

“Kutarajia mashambulizi ya hoja za kisiasa kujibiwa kwa vitisho na mabavu ya vyombo vya dola kama ambavyo imeanza kujengeka katika miaka ya hivi karibuni ni utamaduni wa ovyo.” Amesema na kuongeza;

“Kumtisha, kumdhuru au kumuweka korokoroni mtoa hoja badala ya kuikabili hoja yake si siasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!