Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Magaidi waua 93 Urusi, 4 wadakwa
Habari MchanganyikoKimataifa

Magaidi waua 93 Urusi, 4 wadakwa

Spread the love

Watu takribani 93 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 140 wamejeruhiwa baada ya watu wenye silaha za moto kufyatua risasi katika tamasha la muziki wa rock kwenye ukumbi wa Crocus nje kidogo ya jiji la Moscow jana Ijumaa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Taasisi ya kijasusi ya Urusi (FSB) ilitangaza kuwa moto mkubwa ulilipuka katika jengo hilo na kusababisha sehemu ya paa jirani na eneo la kuchezea kuporomoka.

FSB amemwambia Rais Vladimir Putin kuwa watu wanne kati ya 11 waliohusika katika shambulio katika ukumbi huo, tayari wamekamatwa.

Hata hivyo, Kundi la Islamic State limedai kufanya shambulio hilo, na kwamba waliofanya shambulio walikimbia.

Marekani imesema hakuna sababu ya kutilia shaka madai hayo ya Islamic State, Ikulu ya White House ikisema mapema mwezi huu iliionya Urusi kuhusu uwezekano wa kutokea shambulio kwenye “mikusanyiko mikubwa” jijini Moscow.

Licha ya kwamba Urusi bado haijatoa tamko lolote, Ukraine, ambayo kwa sasa ipo vitani na Urusi, imekana kuhusika kwa namna yoyote.

Picha ya video ambayo BBC imeipata inaonesha washambuliaji wakifyatua risasi ovyo dhidi ya raia waliokuwa wakipiga kelele huku wakijaribu kukimbia na milipuko mingi ikisikika.

Ulinzi umeimarishwa huku matukio ya mikusanyiko yakifutwa kote nchini Urusi wakati maafisa wa ulinzi na usalama wa nchi hiyo wakiwasaka washambuliaji.

Rais Putin bado hajahutubia taifa moja kwa moja, lakini kwa mujibu wa naibu wake amewatakia majeruhi uponaji wa haraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!