Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Mwinyi alikuwa maktaba inayotembea
Habari za SiasaTangulizi

Samia: Mwinyi alikuwa maktaba inayotembea

Spread the love

Rais Samia Suluhu hassan amesema Hayati rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi alikuwa ni maktaba inayotembea na iliyosheheni vitabu vyenye mafunzo ya uadilifu, uzalendo, ustahimilivu, mageuzi, ujasiri, unyenyekevu na uchamungu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika shughuli ya kuaga mwili rais huyo mstaafu wa awamu ya pili leo Jumamosi katika uwanja wa Aman Complex Visiwani Zanzibar, Rais Samia amesema hadhani kama anaweza kuvaa viatu vyake.

 

“Nimeukumbuka msemo wa Kiafrika unaosema anapofariki mzee, maktaba inaungua moto, yaani kila kitu alichonacho mzee anapofariki ni kama maktaba iliyoungua moto kumbukumbu zote zinapotea, mtakubaliana nami kwamba maktaba yetu moja kubwa iliyosheheni hadithi nyingi na nzuri imeungua moto,” amesema Samia.

Hayati Alhaj Ali Hassan Mwinyi anazikwa leo Jumamosi Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Rais huyo wa awamu ya pili alifariki dunia tarehe 29 Februari mwaka huu katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Potofu huzaa potoshi/ potoshi huzaa potofu?

Spread the loveDayosisi 7 za KKKT katika kanda ya Ziwa na Magharibi,...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

error: Content is protected !!