Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Mwinyi alikuwa maktaba inayotembea
Habari za SiasaTangulizi

Samia: Mwinyi alikuwa maktaba inayotembea

Spread the love

Rais Samia Suluhu hassan amesema Hayati rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi alikuwa ni maktaba inayotembea na iliyosheheni vitabu vyenye mafunzo ya uadilifu, uzalendo, ustahimilivu, mageuzi, ujasiri, unyenyekevu na uchamungu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza katika shughuli ya kuaga mwili rais huyo mstaafu wa awamu ya pili leo Jumamosi katika uwanja wa Aman Complex Visiwani Zanzibar, Rais Samia amesema hadhani kama anaweza kuvaa viatu vyake.

 

“Nimeukumbuka msemo wa Kiafrika unaosema anapofariki mzee, maktaba inaungua moto, yaani kila kitu alichonacho mzee anapofariki ni kama maktaba iliyoungua moto kumbukumbu zote zinapotea, mtakubaliana nami kwamba maktaba yetu moja kubwa iliyosheheni hadithi nyingi na nzuri imeungua moto,” amesema Samia.

Hayati Alhaj Ali Hassan Mwinyi anazikwa leo Jumamosi Kijiji kwao Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Rais huyo wa awamu ya pili alifariki dunia tarehe 29 Februari mwaka huu katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!