Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia akabidhi boti 160 za uvuvi, vizimba vya kufugia samaki
Habari za Siasa

Samia akabidhi boti 160 za uvuvi, vizimba vya kufugia samaki

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan ameitaka wizara ya mifugo na uvuvi kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri kudhibiti na kutokomeza vitendo vya uvuvi haramu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumanne wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza baada ya kuzindua na kukabidhi boti za uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kwa wavuvi wa kanda ya ziwa.

Boti za uvuvi

Aidha, Rais Samia ameitaka Wizara hiyo kuwachukulia hatua kali za kisheria wavuvi wanaokiuka taratibu za uvuvi salamna.

Rais Samia pia amesema serikali inafanya jitihada kuinua sekta ya uvuvi nchini kwa kuimarisha utendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili iendane na dhamira ya mageuzi yaliyokusudiwa.

Vile vile, Rais Samia amesema kundi la vijana na wanawake linaongoza kushiriki kwenye ajira zisizo rasmi hivyo serikali inarasimisha shughuli zao kwa kuwawezesha kupata zana na nyenzo za kisasa ili kujikimu kiuchumi.

Vizimba vya kufugia samaki.

Rais Samia amesema serikali imejipanga kukuza sekta ya uvuvi kupitia miradi mbalimbali ikiwemo ununuzi wa meli za kisasa za uvuvi katika bahari kuu, ujenzi wa bandari za uvuvi katika maeneo ya Kilwa Masoko mkoani Lindi na Bagamoyo ili kuongeza pato la taifa.

Boti 160 za uvuvi wa kisasa zimezinduliwa kwa wanufaika 989 pamoja na vizimba 222 vinavyotarajiwa kugaiwa kwa wanufaika 1,213 katika mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu na Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaainisha mpango wa kusaidia wachimbaji wadogo

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa...

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamkaba koo Mo Dewji kwa kutelekeza viwanda vya chai

Spread the loveSERIKALI inakusudia kumuweka kikaangoni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mohammed Enterprises...

error: Content is protected !!