Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia akabidhi boti 160 za uvuvi, vizimba vya kufugia samaki
Habari za Siasa

Samia akabidhi boti 160 za uvuvi, vizimba vya kufugia samaki

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan ameitaka wizara ya mifugo na uvuvi kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri kudhibiti na kutokomeza vitendo vya uvuvi haramu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumanne wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza baada ya kuzindua na kukabidhi boti za uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kwa wavuvi wa kanda ya ziwa.

Boti za uvuvi

Aidha, Rais Samia ameitaka Wizara hiyo kuwachukulia hatua kali za kisheria wavuvi wanaokiuka taratibu za uvuvi salamna.

Rais Samia pia amesema serikali inafanya jitihada kuinua sekta ya uvuvi nchini kwa kuimarisha utendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili iendane na dhamira ya mageuzi yaliyokusudiwa.

Vile vile, Rais Samia amesema kundi la vijana na wanawake linaongoza kushiriki kwenye ajira zisizo rasmi hivyo serikali inarasimisha shughuli zao kwa kuwawezesha kupata zana na nyenzo za kisasa ili kujikimu kiuchumi.

Vizimba vya kufugia samaki.

Rais Samia amesema serikali imejipanga kukuza sekta ya uvuvi kupitia miradi mbalimbali ikiwemo ununuzi wa meli za kisasa za uvuvi katika bahari kuu, ujenzi wa bandari za uvuvi katika maeneo ya Kilwa Masoko mkoani Lindi na Bagamoyo ili kuongeza pato la taifa.

Boti 160 za uvuvi wa kisasa zimezinduliwa kwa wanufaika 989 pamoja na vizimba 222 vinavyotarajiwa kugaiwa kwa wanufaika 1,213 katika mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu na Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!