Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watalii 534,065 waingiza bil. 123 Ngorongoro
Habari Mchanganyiko

Watalii 534,065 waingiza bil. 123 Ngorongoro

Spread the love

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Richard Kiiza amesema kazi kubwa iliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan imeongeza kasi ya watalii wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).


Amesema kutokana na juhudi hizo hadi kufikia mwishoni mwa Desemba 2023 jumla ya watalii 534,065 wametembelea hifadhi hiyo ambapo wageni kutoka nje ni 335,340 na wageni kutoka ndani ya nchi ni 198,725.

Aidha, amesema katika kipindi hicho cha nusu mwaka  zaidi ya Sh 123 bilioni zilikusanywa na kuingia kwenye mfuko mkuu wa Serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari amesema watalii wamekuwa wakitembelea Ngorongoro kwa idadi kubwa na hivyo kuongeza wigo wa mamlaka hiyo kufanya kazi usiku na mchana ili kusimamia juhudi zilizofanywa za kuutangaza utalii.


Aidha, Kamishna Kiiza ametoa wito kwa watanzania kuendelea kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro ili kujionea vivutio mbalimbali ambavyo vipo ndani ya hifadhi na hivyo kutoa fursa kwa wananchi kujifunza kuhusu uhifadhi wa rasilimali za nchi.

Kamishna huyo wa Uhifadhi ameongeza kuwa Uongozi wa NCAA utaendelea kuboresha miundombinu ya utalii ndani ya hifadhi ili kuhakikisha kuwa wageni wote wanaotembelea hifadhi hiyo wanapata huduma nzuri kwa wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!