Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania 2 wafa ajalini Zambia, wengine wajeruhiwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Watanzania 2 wafa ajalini Zambia, wengine wajeruhiwa

Spread the love

RAIA wawili wa Tanzania, watatu wa Zambia na mmoja wa Kenya wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Serenje nchini Zambia, huku watu wengine 42 wakijeruhiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 27 Disemba 2023 na Afisa Mahusiano kwa Umma wa Jeshi la Polisi Zambia, Rae Hamoonga, ajali hiyo ilitokea juzi Jumanne, ikihusisha basi la abiria la Mkombe Luxury, lililokuwa linatokea jijini Johannesburg Afrika Kusini, kuja Dar es Salaam Tanzania kupitia Zambia, pamoja na lori la mizigo.

Ajali hiyo ilitokea mchana wa tarehe 26 Disemba 2023, baada ya basi la abiria kugongana uso kwa uso na lori la mizigo, lililokuwa linatokea Tanzania kwenda Zambia.

Hamoonga ametaja majina ya watu waliopoteza maisha kuwa ni, Davies Kolala (Mzambia), aliyekuwa dereva wa lori la mizigo, Rashid Athumani (Mtanzania), Chibala Abdnegal (Mzambia), Oscar Mwamulima (Mzambia), Ramadhan Abdallah (Mtanzania) na Eunice Jose (Mkenya).

Watoto nane ni miongoni mwa majeruhi 42  wa ajali hiyo, Watanzania waliojeruhiwa walikuwa 14, Wakenya nane, Wazambia 19 na mmo kutoka Uganda.

Taarifa ya Hamoonga imesema majeruhi wanaendelea kutibiwa katika hospitali nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kamati Kuu Chadema kuketi Mei 11

Spread the loveKAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu, Halima Mdee hapatoshi

Spread the loveVITA ya maneno kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha...

Habari Mchanganyiko

Mradi uliotaka kumng’oa madarakani Dk. Mpango waanza majaribio

Spread the loveMRADI wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe, ambao Makamu wa Rais, Dk....

error: Content is protected !!