Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Maisha Burudika Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti
BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni katika uzinduzi wa taasisi ya Professa Jay Foundation pamoja na kuahidi kumgharamia matibabu ya upandikizaji wa figo Muasisi wa taasisi hiyo ambaye pia ni msanii wa Bongofleva, Joseph Haule ‘Profesa Jay’. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Mchango huo umetajwa leo tarehe 11 Desemba 2023 katika hafla ya uzinduzi wa Profesa Jay Foundation iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Akiwasilisha mchango wa Rais Samia, Naibu Waziri wa afya Dk. Godwin Mollel amesema mkuu huyo wa nchi amechangia 50 kwa ajili ya taasisi hiyo.

Pia amesema kama italazimika kwa msanii huyo kupandikizwa figo, atachangia gharama za matibabu hayo.

“Rais Samia ameahidi kuendelea kumsaidia Professa Jay na taasisi yake,’ amesema Dk. Mollel.
Amesema mbali na mchango huo wa Rais, yeye binafsi atachangia kiasi cha Sh milioni sita huku Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akichangia kiasi cha Sh 10 milioni.

Kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mwenyekiti wake Freeman Mbowe ameahidi kuchangia Sh milioni tano, Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Tundu Lissu amechangia Sh milioni mbili, Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika amechangia Sh milioni mbili huku Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho, Godbless Lema akiahidi kuchangia Sh milioni tatu.

Kwa upande wa wasanii akiwamo Ali Kiba na lebal yake ya Kings Music wameahidi kutoa kiasi cha Sh milioni tano na Kundi la Weusi wamechangia kiasi cha Sh milioni moja, Mwanadada Lady Jadee amnechangia Sh milioni mbili, Msanii wa filamu Gabo akishirikiana na Batuli, JB wamechangia Sh milioni mitani huku Chege na Temba (TNC) wakichangia Sh 1.7 Milioni

Kabla ya kuzinduliwa kwa taasisi hiyo inayolenga kuwasaidia watu wenye matatizo ya figo, tayari imeshakusanya ahadi za michango kiasi cha Sh 767 milioni kwa fedha, vifaa tiba na dawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!