Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apangua tena Manaibu Mawaziri, Mnyeti ahamishwa kabla ya kuapishwa
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia apangua tena Manaibu Mawaziri, Mnyeti ahamishwa kabla ya kuapishwa

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya
uhamisho na uteuzi wa viongozi mbalimbali ikiwamo Naibu Waziri David Silinde ambaye amehamishwa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenda kuwa Naibu Waziri wa Kilimo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Sakaam …(endelea).

Aidha, Alexander Mnyeti ambaye mapema leo ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, jioni hii amehamishiwa katika nafasi ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi.

Katika taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu leo Jumatano jioni, pia Rais Samia amemteua Balozi Mhandisi Aisha Amour kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi.

Katika taarifa hiyo pia ameteua Wajumbe wanne wa Tume ya Mipango.

Wajumbe hao ni Balozi Ombeni Yohana Sefue – Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu na Omar Issa – Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela.

Wengine ni Balozi Ami Ramadhan Mpungwe – Balozi Mstaafu na Mịasiriamali na Maryam Salim- Mencja Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Cambodia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Potofu huzaa potoshi/ potoshi huzaa potofu?

Spread the loveDayosisi 7 za KKKT katika kanda ya Ziwa na Magharibi,...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

error: Content is protected !!