Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mikoa 16 kupata umeme kwa mgawo kuanzia leo
Habari MchanganyikoTangulizi

Mikoa 16 kupata umeme kwa mgawo kuanzia leo

Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO)  limetangaza kuzimwa kwa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovoti 220 Kidatu -Kihansi kwa tarehe 26 hadi 28 Agosti 2023

kuanzia saa moja kamili asubuhi hadi saa 12 kamili jioni (01:00 -12:00). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa na shirika hilo imetaja sababu ya kuzimwa kwa njia hiyo kuwa ni kuruhusu Mkandarasi anayejenga kituo kipya cha kupoza umeme Ifakara kuunganisha kituo hicho kwenye gridi ya Taifa.

Imesema kazi hiyo itahusisha kuunga njia ya msongo wa Kilovoti 220 Kihansi -Kidatu kwenye kituo kipya.

“Kuunganishwa kwa kituo hiki kipya ni muhimu kwani kutasaidia kuongeza ubora na upatikanaji wa umeme katika wilaya za Kilombero, Ulanga na maeneo ya jirani sambamba na kuvutia wawekezaji,” imesema.

Taarifa hiyo imesema, kutokana na kazi hii baadhi ya maeneo kwenye mikoa yataathirika kwa awamu katika nyakati tofauti, ratiba kamili itatolewa kwenye Mikoa ya Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Songwe, Dodoma, Singida, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Mwanza, Geita na Mara.

“Tutaendelea kuwafahamisha maendeleo ya kazi hiyo hadi kukamilika kwake,” imesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafugaji kuku Ihemi wanufaika na mafunzo

Spread the loveWADAU  wa mnyororo wa thamani katika sekta ndogo ya kuku...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaainisha mpango wa kusaidia wachimbaji wadogo

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa...

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

error: Content is protected !!