Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mikoa 16 kupata umeme kwa mgawo kuanzia leo
Habari MchanganyikoTangulizi

Mikoa 16 kupata umeme kwa mgawo kuanzia leo

Spread the love

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO)  limetangaza kuzimwa kwa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovoti 220 Kidatu -Kihansi kwa tarehe 26 hadi 28 Agosti 2023

kuanzia saa moja kamili asubuhi hadi saa 12 kamili jioni (01:00 -12:00). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa na shirika hilo imetaja sababu ya kuzimwa kwa njia hiyo kuwa ni kuruhusu Mkandarasi anayejenga kituo kipya cha kupoza umeme Ifakara kuunganisha kituo hicho kwenye gridi ya Taifa.

Imesema kazi hiyo itahusisha kuunga njia ya msongo wa Kilovoti 220 Kihansi -Kidatu kwenye kituo kipya.

“Kuunganishwa kwa kituo hiki kipya ni muhimu kwani kutasaidia kuongeza ubora na upatikanaji wa umeme katika wilaya za Kilombero, Ulanga na maeneo ya jirani sambamba na kuvutia wawekezaji,” imesema.

Taarifa hiyo imesema, kutokana na kazi hii baadhi ya maeneo kwenye mikoa yataathirika kwa awamu katika nyakati tofauti, ratiba kamili itatolewa kwenye Mikoa ya Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Songwe, Dodoma, Singida, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Mwanza, Geita na Mara.

“Tutaendelea kuwafahamisha maendeleo ya kazi hiyo hadi kukamilika kwake,” imesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!