Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Watoto 500 wafariki kwa njaa
Kimataifa

Watoto 500 wafariki kwa njaa

Spread the love

SHIRIKA la kimataifa la hisani la Save the Children limesema takriban watoto 500 wamefariki kutokana na njaa nchini Sudan. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Shirika hilo kati ya watoto hao 500 pia wapo watoto zaidi ya 20 katika kituo cha watoto yatima kinachosimamiwa na serikali katika mji mkuu Khartoum, tangu mapigano yalipozuka nchini humo mwezi Aprili mwaka huu.

Shirika la Save the Children pia lilisema kuwa karibu watoto 31,000 wanakosa huduma ya lishe na matibabu ya utapiamlo tangu shirika hilo la misaada kusitisha shughuli zake kwenye vituo 57 vya lishe nchini Sudan.

Mzozo huo wa Sudan umegeuza jiji la Khartoum na maeneo mengine ya mijini kuwa viwanja vya vita. Wakazi wengi wanaishi bila maji na umeme, na mfumo wa huduma za afya nchini humo umeporomoka.

Mkurugenzi wa shirika la Save the Children nchini Sudan, Arif Noor amesema hawakutegemea kuwaona idadi kubwa ya watoto kama hao wakifa kwa njaa.

Noor amesema mbali na watoto hao kufa njaa idadi ya watoto walioachishwa shule nchini humo pia imeongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!