Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango: Siri ndiyo uhai wa Serikali
Habari za Siasa

Dk. Mpango: Siri ndiyo uhai wa Serikali

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango
Spread the love

 

MAKAMU wa Rais nchini Tanzania, Dk. Philip Mpango, amewataka Wakuu wa Wilaya kote nchini kudhibiti uvujaji wa siri za serikali kwa kuepuka kutuma nyaraka za Serikali kwenye mitandao ya kijamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Dk. Mpango amesisitiza kuwa Wakuu hao wa Wilaya wanapaswa kuzingatia kuwa “siri ndiyo uhai wa Serikali.”

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 13 Machi 202, wakati akifungua mafunzo ya siku sita kwa Wakuu wa Wilaya yanayoendelea jijini Dodoma.

“Jambo la pili mtakuwa na mada kuhusu utunzanji wa siri za Serikali, jambo hili ni kuhimu sana hasa katika kipindi cha utandawazi na matumizi ya mitandao ya kijamii kwahiyo itawapasa mzingatie kuwa siri ndiyo uhai wa serikali hivyo ni lazima kudhibiti uvujaji wa siri za Serikali, epukeni kabisa kuitumia mitandao ya kijamii kama vile Whatsapp na email binafsi kutuma nyaraka za Serikali,” amesema Dk. Mpango.

Aidha Dk. Mpango amesisitiza kuhusu matumizi ya walinzi na waandishi wa habari binafsi na kusema kuwa upo utaratibu wakufuata endapo itabainika kiongozi anahitaji watumishi hao.

Amesema viongozi kujipatia watumishi hao bila kufuata taratibu za Serikali kuna hataraisha usalama wao na hata wa siri za Serikali.

“Kumekuwepo watu wanajichukulia walinzi binafsi na waandishi wa habari binafsi katika ofisi za umma, sasa zipo taratibu za kufuta endapo itabainika kiongozi anahitaji kupatiwa wasaidizi wa aina hii kwahiyo zinagatieni taratibu zilizopo na si vinginevyo,” amesisitiza.

Vilevile amewataka Wakuu wa Wilaya ambao pia ni Wenyeviti wa Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya, kuwa makini na maneno wanayozungumza na wasaidizi wao hususani madereva na watu wengine wanapokuwa nje ya ofisi hata sehemu za starehe ili kuepuka kutoa siri za Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!