Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango: Siri ndiyo uhai wa Serikali
Habari za Siasa

Dk. Mpango: Siri ndiyo uhai wa Serikali

Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango
Spread the love

 

MAKAMU wa Rais nchini Tanzania, Dk. Philip Mpango, amewataka Wakuu wa Wilaya kote nchini kudhibiti uvujaji wa siri za serikali kwa kuepuka kutuma nyaraka za Serikali kwenye mitandao ya kijamii. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Dk. Mpango amesisitiza kuwa Wakuu hao wa Wilaya wanapaswa kuzingatia kuwa “siri ndiyo uhai wa Serikali.”

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 13 Machi 202, wakati akifungua mafunzo ya siku sita kwa Wakuu wa Wilaya yanayoendelea jijini Dodoma.

“Jambo la pili mtakuwa na mada kuhusu utunzanji wa siri za Serikali, jambo hili ni kuhimu sana hasa katika kipindi cha utandawazi na matumizi ya mitandao ya kijamii kwahiyo itawapasa mzingatie kuwa siri ndiyo uhai wa serikali hivyo ni lazima kudhibiti uvujaji wa siri za Serikali, epukeni kabisa kuitumia mitandao ya kijamii kama vile Whatsapp na email binafsi kutuma nyaraka za Serikali,” amesema Dk. Mpango.

Aidha Dk. Mpango amesisitiza kuhusu matumizi ya walinzi na waandishi wa habari binafsi na kusema kuwa upo utaratibu wakufuata endapo itabainika kiongozi anahitaji watumishi hao.

Amesema viongozi kujipatia watumishi hao bila kufuata taratibu za Serikali kuna hataraisha usalama wao na hata wa siri za Serikali.

“Kumekuwepo watu wanajichukulia walinzi binafsi na waandishi wa habari binafsi katika ofisi za umma, sasa zipo taratibu za kufuta endapo itabainika kiongozi anahitaji kupatiwa wasaidizi wa aina hii kwahiyo zinagatieni taratibu zilizopo na si vinginevyo,” amesisitiza.

Vilevile amewataka Wakuu wa Wilaya ambao pia ni Wenyeviti wa Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya, kuwa makini na maneno wanayozungumza na wasaidizi wao hususani madereva na watu wengine wanapokuwa nje ya ofisi hata sehemu za starehe ili kuepuka kutoa siri za Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!