Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yavuna wanachama wa CUF, CCM, Chadema Zanzibar
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yavuna wanachama wa CUF, CCM, Chadema Zanzibar

Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimeendelea kuvuna wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) baada ya kuwapokea 305 kupitia mkutano wake wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Tibirinzi, kisiwani Pemba, Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, wanachama hao wamejiunga na chama hicho leo tarehe 4 Machi 2023, katika mkutano huo uliofanyika visiwani Zanzibar.

Mbali na wanachama hao wa CUF, taarifa ya Shaibu imesema ACT-Wazalendo imepokea wanachama 10 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mmoja kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kupitia taarifa hiyo, Shaibu amesema kundi la wanachama hao liliongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF Zanzibar, Abbas Juma Muhunzi.

“Chama cha ACT Wazalendo, kwenye Mkutano wake Kisiwani Pemba uliofanyika katika viwanja vya Tibirinzi leo tarehe 04 Feb kimewapokea wanachama 305 wa CUF, 10 wa CCM na mmoja wa Chadema wakiongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF Zanzibar Ndugu Abbas Juma Muhunzi,” imesema taarifa ya Shaibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!