CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimeendelea kuvuna wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) baada ya kuwapokea 305 kupitia mkutano wake wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Tibirinzi, kisiwani Pemba, Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, wanachama hao wamejiunga na chama hicho leo tarehe 4 Machi 2023, katika mkutano huo uliofanyika visiwani Zanzibar.
Mbali na wanachama hao wa CUF, taarifa ya Shaibu imesema ACT-Wazalendo imepokea wanachama 10 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mmoja kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Kupitia taarifa hiyo, Shaibu amesema kundi la wanachama hao liliongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF Zanzibar, Abbas Juma Muhunzi.
“Chama cha ACT Wazalendo, kwenye Mkutano wake Kisiwani Pemba uliofanyika katika viwanja vya Tibirinzi leo tarehe 04 Feb kimewapokea wanachama 305 wa CUF, 10 wa CCM na mmoja wa Chadema wakiongozwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF Zanzibar Ndugu Abbas Juma Muhunzi,” imesema taarifa ya Shaibu.
Leave a comment