Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Mwinyi ataja mikakati kushusha bei ya mafuta Zanzibar
Habari Mchanganyiko

Rais Mwinyi ataja mikakati kushusha bei ya mafuta Zanzibar

Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi , amesema Serikali yake inakusudia kuboresha miundombinu ya bandari pamoja na hifadhi ya kutosha ya mafuta, ili kushusha bei yake inayotokana na kuhifadhiwa nje ya visiwa hivyo. Anaripoti Mwandishi Wetyu, Zanzibar … (endelea).

Rais Mwinyi ametoa taarifa hiyo leo tarehe 4 Machi 2023, akizindua Bohari ya Mafuta katika Bandari ya Mangapwani, visiwani Zanzibar.

Amesema uboreshwaji wa maeneo hayo utapelekea mafuta kusafirishwa moja kwa moja kutoka sokoni hadi Zanzibar, kitendo kitakachopunguza gharama za uhifadhi na usafirishaji.

“Kwa hali ya sasa Zanzibar hatuleti mafuta moja kwa moja, yakitoka Dar es Salaam yanahifadhiwa Tanga sababu hapa hatuna hifadhi ya kutosha, yakitoka Tanga yanaletwa Zanzibar. Haya yote yanasababisha mafuta kuwa na bei hii,” amesema Rais Mwinyi na kuongeza:

“ Nini tunataka kufanya, tukishakuwa na hifadhi ya kutosha na gati ya kutosha, meli moja kwa moja itashusha Zanzibar, tutakuwa na mafuta bei rahisi. Na huo ndiyo mpango na azma ya Serikali, tutafanya kila linalowezekana hilo litimie na maslahi ya nchi kwenda mbele.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!