Tuesday , 14 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sangoma afariki akirusha roho na mke wa Mchungaji gesti
Habari Mchanganyiko

Sangoma afariki akirusha roho na mke wa Mchungaji gesti

Spread the love

MGANGA mmoja wa kienyeji amepoteza fahamu na kufariki wakati akidaiwa kurushana roho na mke wa mchungaji katika hoteli moja huko Ikere, jimbo la Ekiti nchini Nigeria. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Gazeti la The Punch liliripoti kuwa kisa hicho kilitokea tarehe 2 Januari 2023 wakati mke wa mchungaji na mganga huyo walipokutana.

Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye hakutaka kutajwa jina alithibitisha kuwa mwanamke huyo alikuwa mke wa mchungaji. “Mwanaume huyo alifariki dunia katika chumba cha hoteli alipokuwa akifanya mapenzi na mwanamke huyo. Mwanamke huyo alianza kupiga mayowe kuomba msaada,” alisema.

Kwa mujibu wa shahidi huyo, meneja wa hoteli hiyo na baadhi ya wakazi walikimbilia eneo la tukio na mara moja wakampeleka mtu huyo katika hospitali ya karibu ila alipofika alikuwa amekata roho tayari.

Akizungumzia mkasa huo Msemaji wa polisi huko Ekiti, Sunday Abutu alisema tukio hilo kwa sasa linachunguzwa. Alifichua kifo cha mganga huyo kilithibitishwa na kamanda wa polisi wa jimbo la Ekiti tarehe 2 Januari 2023.

“Tunaweza kuthibitisha kifo cha mwanamume huyo kilichotokea katika hoteli moja huko Ikere Ekiti siku ya Jumatatu. Mwili wake ulichukuliwa na kuhifadhiwa katika makafani,” msemaji wa polisi alisema.

Aliongeza kuwa wanamhoji mwanamke huyo huku wakiendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo cha mwanamume huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CUF yajipanga kuelekea chaguzi zijazo

Spread the loveCHAMA cha Wananchi (CUF), kimejipanga kujijenga kisiasa kuelekea chaguzi zijazo...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yatoa vifaa tiba hospitali ya Mpitimbi Songea

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imetoa misaada ya vifaa...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yaongoza kikao cha wataalamu Afrika kuhusu nishati safi ya kupikia

Spread the loveTanzania imeongoza kikao cha wataalamu kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Moduli ya kuwasilisha rufaa za zabuni kieletroniki kuanza Julai

Spread the loveMamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imesema moduli...

error: Content is protected !!