RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwamo Emanuel Mpawe Tutuba kuwa Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Tutuba ambaye alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango amechukua nafasi ya Profesa Florence Luoga ambaye amemaliza muda wake.
Katika taarifa iliyotolewa leo tarehe 7 Januari, 2023 imeonesha pia amemteua Dk. Natu El Maamry Mwamba kuwa Katibu Mkuu wizara ya Fedha na Mipango akichukua nafasi ya Tutuba.
Dk. Mwamba alikuwa mhadhiri mwandamizi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni ya uendeshaji wa kiwanja wa ndege Kilimanjaro (KADCO).
Leave a comment