Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rungwe: Tumekula ubwabwa na kuanza mwaka kwa faraja tupu!
Habari za Siasa

Rungwe: Tumekula ubwabwa na kuanza mwaka kwa faraja tupu!

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chaumma
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Taifa, Hashim Rungwe amesema hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza kuondoa zuio la mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa kwao wapinzani ni faraja tupu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rungwe ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Januari, 2023 Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kuhudhuria mkutano ulioitishwa na Rais Samia dhidi ya viongozi wa vyama 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu.

Katika mkutano huo mbali na Rais Samia kutangaza kufuta zuio hilo la mikutano ya hadhara, pia ametangaza kuanza kwa mchakato wa marekebisho ya sheria mbalimbali ikiwamo ya uchaguzi na vyama vya siasa pamoja na kuanza mchakato wa namna ya kuondoa mkwamo wa Katiba mpya.

Akizungumzia hatua hiyo, Rungwe amesema; “Tumeanza mwaka kwa tangazo zuri, sana, tumekuja kwa rais tumekula ubwabwa kwanza na kupata matangazo yake yaliyosheheni faraja kwamba tutakwenda kufanya mikutano ya hadhara bila vizuizi.

“Ni jambo la kufurahisha sana, tumeondoka zile zama za kutishana, nafikiri ni jambo jema, tunakwenda kwenye vitendo ili tuone kwani polisi wameelezwa vyake na sisi tumeelewa vyetu.

“Pongezi sana kwa rais na hii siku tulikuwa tunaisubiria sana. tuwe huru tuondokane na zile zama za kwamba … mimi nimeshasema!” alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba mbali na kupongeza hatua hiyo, alisisitiza kuwa yale yanayohitaji kuundiwa kamati maalumu pamoja na marekebisho ya sheria, yasichukue muda mrefu hasa ikizingatiwa mwaka 2024 kuna uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

error: Content is protected !!