BENKI ya Exim Tanzania imeendelea kugawa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu na simu janja (smartphones) kwa washindi wa kampeni yake “Chanja Kijanja, Kimasta Zaidi’’ inayolenga kuhamasisha wateja wa benki ya Exim kutumia kadi zao za Mastercard katika manunuzi ya mtandaoni au kufanya malipo kupitia mashine za malipo (POS) katika maduka mbalimbali na maeneo mengine nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kampeni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi Novemba inatoa fursa kwa wateja wa benki hiyo wanaotumia kadi zao za Exim Mastercard kufanya miamala, kuwa kwenye nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu, Simu janja (Smart Phones) na safari zilizolipiwa gharama zote kwenda mapumziko katika mataifa ya Dubai, Uturuki na Afrika Kusini wao pamoja na wenza wao.
Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo kwa washindi hao ikiwemo zawadi ya simu janja aina ya Iphone 14 Pro kwa mshindi wa mwezi ambae ni Emanuel Lutambi mkazi wa mkoa wa Iringa, Afisa Idara ya Huduma Mbadala Kupitia Mifumo ya Kidigitali wa Benki ya Exim, Gregory Malembeka alisema hadi kufikia sasa zaidi ya washindi 100 wameshajishindia zawadi ya fedha kiasi cha Tsh 100,000 kila mmoja kupitia droo “bahati nasibu” na mitandao.
“Inafahamika kwamba kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka kinahusisha manunuzi zaidi kutokana na sherehe na sikukuu ya Christmas. Wito wetu kwa wateja wetu ni wao kufanya manunuzi kwa kutumia Exim Mastercard iwe mtandaoni au kwenye mashine za malipo (POS) ili waweze kujiweka kwenye nafasi ya kushinda kwa kuwa zawadi bado ni nyingi.’’
“Ifahamike kwamba unapochanja au kulipia bidhaa au huduma basi unajiweka kwenye nafasi ya kuingia kwenye droo ya kushinda safari zilizolipiwa kila kitu kikamilifu kwa siku tano kwenda Dubai, Uturuki au Afrika Kusini pamoja na mpendwa wako. Pia unaweza kuwa mshindi wa iPhone 14 pro inayotoka kila mwezi au pesa taslimu100,000 inayotoka kila wiki….ujanja ni kuchanja tu na Exim Mastercard,” alisema.
Leave a comment