Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makundi CCM yamchefua Dk. Samia
Habari za Siasa

Makundi CCM yamchefua Dk. Samia

Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanachama wa chama hicho kuacha kujenga nyufa ndani ya chama baada ya chaguzi kukamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dkt Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Disemba, 2022 mkoani Dodoma katika siku ya pili na ya mwisho ya mkutano mkuu wa 10 wa CCM.

Amesema ndani ya CCM bado kuna makundi ambayo yanaendeleza nongwa hata baada ya kumalizika kwa chaguzi hizo.

Dk. Samia amesema makundi hayo hayajengi chama na badala yake yanakidhoofisha na kukifanya kushindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Amesema anapenda kukiona Chama Cha Mapinduzi kikiendelea kuwa chama na chombo madhubuti cha kufuta unyonyaji wa aina zote na kupambana na jaribio lolote la uonevu.

Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa pia amekumbusha majukumu ya chama hicho kuwa ni pamoja na kuisimamia serikali ili iweze kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!