RAIS wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amesema amekusudia kufanya mabadiliko ya baadhi ya viongozi wa Serikali ili kuachana na viongozi ambao wanashindwa kuendana na kasi yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Dk Samia amesema hayo leo tarehe 8 Disemba 2022 katika Mkutano wa 10 wa chama hicho ambao leo umefikia tamatu mkoani Dodoma.
Amesema kuwa bado wanasafari ya miaka mitatu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2025, ili wananchi wawe mashuhuda wa yanayofanywa.
“Kubwa zaidi tunapokwenda kwa wananchi, ni wananchi wenyewe wanayosema serikali waliyofanya kwao, tofauti na utamaduni tuliokuwa nao nyuma, kwamba tunapokwenda kwa wananchi serikali ndio tunawaambiwa tumewafanyia, wakati mwingine wanashangaa hiki kimefanyika wapi,” amesema Dk. Samia.
Amesema mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa wananchi kuona na kutoa tathmini ya yaliyofanyika na wenyewe kuwa mashuhuda wa kila kinachofanyika.
Leave a comment