RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema Katibu Mkuu mstaafu wa chama hicho, Yusuph Makamba aliteleza ulimi ndio maana akasema kwamba ‘wazuri hawafi’. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Marekebisho hayo ya Rais Samia yamekuja siku moja baada ya mjadala mkali kuibuka miongoni mwa Watanzania katika mitandao ya kijamii kuhusu kauli ya Mzee Makamba alipomueleze Dk. Samia kuwa asiogope kufa kwa sababu wazuri hawafi.
Aidha, akitoa hotuba ya kufunga mkutano wa 10 wa chama hicho uliofanyika leo tarehe 8 Disemba, 2022 jijini Dodoma, Rais Samia ameongeza kuww Mzee Makamba alikuwa kwenye ‘emotion’.
“Katika dhana ya kujikosoa na kujisahihisha naomba kurekebisha ulimi ulioteleza wa kaka yangu Mzee Makamba kwamba wakati ananisifia alisema ‘usiogope hutokufa…mtu mzuri hafi.’
“Hajakusudia kwamba wanaokufa ni watu wabaya… wote hapa tumefiwa na baba na mama na ndugu, wote ni wapenzi wetu.
Kwa hiyo nirekebishe ili kipengele kile kisiende kutumika vibaya.
“Mzee alikuwa kwenye emotion, alidhani amenikosea aliponiambia si utakufa utatupisha! lakini akajirudisha akaniambia usijali mtu mzuri hafi. Alikuwa kwenye emotiona lakini hajakusudia vingine vyovyote,” amesema Rais Samia ambaye jana amechaguliwa rasmi kwa kupigiwa kura na wajumbe wa mkutano huo kuwa mwenyekiti wa kwanza mwanamke wa CCM.
Leave a comment