Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Samia aomba radhi kauli ya Mzee Makamba ‘wazuri hawafi’
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Samia aomba radhi kauli ya Mzee Makamba ‘wazuri hawafi’

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema Katibu Mkuu mstaafu wa chama hicho, Yusuph Makamba aliteleza ulimi ndio maana akasema kwamba ‘wazuri hawafi’. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma  …  (endelea).

Marekebisho hayo ya Rais Samia yamekuja siku moja baada ya mjadala mkali kuibuka miongoni mwa Watanzania katika mitandao ya kijamii kuhusu kauli ya Mzee Makamba alipomueleze Dk. Samia kuwa asiogope kufa kwa sababu wazuri hawafi.

Aidha, akitoa hotuba ya kufunga mkutano wa 10 wa chama hicho uliofanyika leo tarehe 8 Disemba, 2022 jijini Dodoma, Rais Samia ameongeza kuww Mzee Makamba alikuwa kwenye ‘emotion’.

“Katika dhana ya kujikosoa na kujisahihisha naomba kurekebisha ulimi ulioteleza wa kaka yangu Mzee Makamba kwamba wakati ananisifia alisema ‘usiogope hutokufa…mtu mzuri hafi.’

“Hajakusudia kwamba wanaokufa ni watu wabaya… wote hapa tumefiwa na baba na mama na ndugu, wote ni wapenzi wetu.
Kwa hiyo nirekebishe ili kipengele kile kisiende kutumika vibaya.

“Mzee alikuwa kwenye emotion, alidhani amenikosea aliponiambia si utakufa utatupisha! lakini akajirudisha akaniambia usijali mtu mzuri hafi. Alikuwa kwenye emotiona lakini hajakusudia vingine vyovyote,” amesema Rais Samia ambaye jana amechaguliwa rasmi kwa kupigiwa kura na wajumbe wa mkutano huo kuwa mwenyekiti wa kwanza mwanamke wa CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!