Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makundi CCM yamchefua Dk. Samia
Habari za Siasa

Makundi CCM yamchefua Dk. Samia

Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanachama wa chama hicho kuacha kujenga nyufa ndani ya chama baada ya chaguzi kukamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dkt Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Disemba, 2022 mkoani Dodoma katika siku ya pili na ya mwisho ya mkutano mkuu wa 10 wa CCM.

Amesema ndani ya CCM bado kuna makundi ambayo yanaendeleza nongwa hata baada ya kumalizika kwa chaguzi hizo.

Dk. Samia amesema makundi hayo hayajengi chama na badala yake yanakidhoofisha na kukifanya kushindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Amesema anapenda kukiona Chama Cha Mapinduzi kikiendelea kuwa chama na chombo madhubuti cha kufuta unyonyaji wa aina zote na kupambana na jaribio lolote la uonevu.

Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa pia amekumbusha majukumu ya chama hicho kuwa ni pamoja na kuisimamia serikali ili iweze kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!