Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mshindi wa Promosheni ya NMB MastaBata KoteKote akabidhiwa Pikipiki Mwanza
Habari Mchanganyiko

Mshindi wa Promosheni ya NMB MastaBata KoteKote akabidhiwa Pikipiki Mwanza

Spread the love

MSIMU wa nne wa promosheni ya NMB MastaBata kwa ajili ya kuchagiza matumizi ya kadi za malipo za kidijitali umezidi kunoga baada ya kundi la kwanza la washindi 51 wa kila mwezi kupatikana katika droo iliyofanyika kwenye tawi la NMB Kenyatta mkoani Mwanza wiki hii, ambapo 49 walijishindia pesa taslimu TZS 1,000,000 kila mmoja na wawili wakishinda pikipiki aina ya Boxer. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lengo la kampeni hii ya MastaBata KoteKote ni kuhamasisha matumizi ya kadi ya NMB Mastercard na Lipa Mkononi (Mastercard QR) kwa wateja wa NMB wanapofanya malipo kwenye manunuzi yao.

Akizungumzia zawadi hiyo, Mkazi wa Bunda jijini Mara, Bernard Lucas Matiku alisema ‘Asante sana Benki yangu ya NMB kwa kunizawadia pikipiki, nimeanza vizuri msimu huu wa sikukuu maana sasa sina wasiwasi kuendesha mishe zangu’ baada ya kukabidhiwa pikipiki aliyoshinda katika promotion ya NMB MastaBata KoteKote.

Mshindi wa Kampeni ya MastaBata KoteKote, Bernard Matiku (kulia) akipokea funguo ya pikipiki kutoka kwa Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa – Baraka Ladislaus wakati wa hafla ya kukabidhiwa. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Biashara ya kadi wa NMB – Philbert Casmir.

Aidha, Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa – Baraka Ladislaus  alisema zoezi hilo lililosimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania limepelekea idadi ya washindi wa kampeni ya NMB MastaBata KoteKote kufikia 225 hadi sasa.

Alisema zawadi walizoshinda wateja hao kwa siku hii zina thamani ya zaidi ya TZS milioni 55 huku shindano zima likiwa na thamani ya zaidi ya TZS milioni 300.

Naye Mkuu wa Idara ya Biashara ya Kadi wa NMB- Philbert Casmir alisema zawadi za kila wiki zitakuwepo ambapo jumla ya washindi 75 watanyakua pesa taslimu TZS 100,000 kila mmoja na mmoja zawadi ya Pikipiki (boxer).

Mshindi wa Kampeni ya MastaBata KoteKote, Bernard Matiku(wa pili kushoto) akibonyeza kitufe ili kuwapata washindi wengine wa kampeni hiyo. Wakishuhudia; Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Biashara ya Kadi wa NMB- Philbert Casmir, Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa – Baraka Ladislaus(wa tatu kushoto) na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya kubahatisha – Erick Mremi(kulia).

Alisema kwa mwezi jumla ya washindi 98 watanyakua pesa taslimu TZS 1,000,000 kila mmoja huku kila mwezi kukiwepo zawadi ya Pikipiki (Boxer) mbili. Zawadi ya droo ya mwisho ni safari ya siku nne huko Dubai kwa washindi saba na wenza wao.

“Endelea kufanya malipo kwa kutumia NMB mastercard au Lipa Mkononi (mastercard QR) ujiwekee nafasi ya kushindia zawadi kibao na #NMBMastaBataKoteKote,” alisema,

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!