Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Wananchi jipindeni kufanya kazi
Habari za Siasa

Samia: Wananchi jipindeni kufanya kazi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa Watanzania kujipinda kufanya kazi ili mapato yapatikane kusukuma gurudumu la maendeleo ya Taifa hasa ikizingatiwa mapato yayanayopatikana ni madogo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Samia ametoa rai hiyo leo tarehe 22 Novemba, 2022 aliposimama kuzungumza na wananchi wa Kondoa – Dodoma wakati akielekea Manyara na Arusha.

Amesema hakuna kazi zilizosimama na kazi inaendelea kwenye sekta zote Tanzania

“Tunaomba wakati serikani inajipinda kufanya kazi wananchi nanyi jipindeni kufanya kazi, anayelima alime, anayevua avue, anayechimba achimbe wote tufanye kazi tupate mapato nchi yetu iende mbele, nchi yetu ni kubwa lakini mapato ni madogo ila hayohayo tunayopata tunagawana hapa na pale,” amesema.

Amesema Serikali imejitahidi kushusha fedha kwa wananchi na katika sekta mbalimbali na huo ndio mwenendo Serikali hiyo anayoiongoza kwa sasa.

“Mwananchi kwanza sisi huku juu baadae… tutajijua tutakavyoishi. Ndio maana tunashusha fedha nyingi zije zitoe huduma kwa wananchi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!