Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Wananchi jipindeni kufanya kazi
Habari za Siasa

Samia: Wananchi jipindeni kufanya kazi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa Watanzania kujipinda kufanya kazi ili mapato yapatikane kusukuma gurudumu la maendeleo ya Taifa hasa ikizingatiwa mapato yayanayopatikana ni madogo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Samia ametoa rai hiyo leo tarehe 22 Novemba, 2022 aliposimama kuzungumza na wananchi wa Kondoa – Dodoma wakati akielekea Manyara na Arusha.

Amesema hakuna kazi zilizosimama na kazi inaendelea kwenye sekta zote Tanzania

“Tunaomba wakati serikani inajipinda kufanya kazi wananchi nanyi jipindeni kufanya kazi, anayelima alime, anayevua avue, anayechimba achimbe wote tufanye kazi tupate mapato nchi yetu iende mbele, nchi yetu ni kubwa lakini mapato ni madogo ila hayohayo tunayopata tunagawana hapa na pale,” amesema.

Amesema Serikali imejitahidi kushusha fedha kwa wananchi na katika sekta mbalimbali na huo ndio mwenendo Serikali hiyo anayoiongoza kwa sasa.

“Mwananchi kwanza sisi huku juu baadae… tutajijua tutakavyoishi. Ndio maana tunashusha fedha nyingi zije zitoe huduma kwa wananchi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!