Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kimbunga Ian chasababisha dhoruba kubwa kuwahi kutokea Marekani
Kimataifa

Kimbunga Ian chasababisha dhoruba kubwa kuwahi kutokea Marekani

Spread the love

KIMBUNGA Ian kimetokea Florida  nchini Marekani na kusababisha madhara makubwa ikiwemo mafuriko. Anaripoti Helena Mkonyi TUDARCo, kwa msaada wa vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea).

Vyombo vya habari nchini humo viliripoti kwamba miti na magari yalionekana yakisombwa na maji na baadhi ya nyumba sehemu mbalimbali ziliathiriwa ikiwemo ni pamoja na kukosekana kwa umeme.

Ian kilitua Jumatano Kusini-Magharibi mwa Florida, Wataalamu wa hali ya hewa nchini humo wamesema kuwa Kimbunga hicho kimeleta dhoruba zenye nguvu zaidi kuwai kurekodiwa Marekani.

Wanasema “dhoruba hiyo ya kiwango cha nne, ilitua karibu na Cayo Costa, Kisiwa kilichohifadhiwa Magharibi mwa Fort Myers, kikiwa na kasi ya kilomita 241 kwa saa, kikielekea Kaskazini-Mashariki mwa Pensula ya Kaskazini-Magharibi.”

Aidha serikali ya Jimbo la Florida na Marekani awali zilitoa tahadhari kwa wakazi wa maeneo yaliyolengwa na dhoruba hiyo, huku wakazi wengi wakilazimika kuondoka kwenye makazi yao kwa usalama wao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!